• Seynation Updates

    Saturday 9 January 2016

    MSISIMKO WA WATANZANIA KUFUATIA USHINDI WA MBWANA SAMATA

    Mashabiki wa soka nchini Tanzania na nyingine za eneo la Afrika Mashariki wamepokea kwa furaha ushindi wa Mtanzania Mbwana Ally Samatta kuwa mchezaji bora wa mwaka anayechezea barani Afrika.

    Samatta baadaye aliweka kwenye Twitter picha hii inayomuonyesha akiwa na tuzo yake na akiwa amejifunika kwa shiti yenye rangi za bendera ya Tanzania.

    Akizungumza baada ya kutangazwa mshindi, Samatta alisema: "Najivunia sana kushinda tuzo muhimu sana kiasi hiki. Naijionea fahari na kuonea fahari taifa langu pia. Natoka taifa (Tanzania) ambalo si moja ya mataifa makubwa katika soka Afrika. Kutawazwa kuwa mchezaji bora Afrika, ni jambo kubwa sana kwangu."

    No comments:

    Post a Comment

    VIDEO MPYA

    UMBEA MTUPUU

    MAPENZI