• Seynation Updates

    Tuesday 5 April 2016

    Siku moja baada ya Antonio Conte kutangazwa kuwa kocha wa Chelsea, yameandikwa haya ya kufungiwa miezi sita

    Ni siku moja baada ya uongozi wa Chelsea ya Uingereza kutangaza kumpa mkataba wa miaka mitatu kocha wa timu ya taifa ya Italia Antonio Conte ambaye atajiunga na klabu yao mwishoni mwa msimu. Leo April 5 Antonio Conteameripotiwa kuwa, huenda akafungwa miezi sita.
    Muendesha mashtaka Roberto Di Martino kutoka Italiaanaripotiwa na Sky Sports kuwa April 5 2016 ameendeleza shauri la Conte kutuhumiwa kwa upangaji wa matokeo ya mechi ya ushindi wa Siena wa goli 1-0 dhidi ya AlbinoleffeMay 2011 na sare ya goli 2-2 dhidi ya Novara May 2011.
    conte-antonio-conte-antonio_3443206
    Antonio Conte
    Kama Antonio Conte atakutwa na hatia huenda akakutana na kifungo cha miezi sita, Conte alituhumiwa kujihusisha na upangaji wa matokeo msimu wa 2010-2011 wakati akiwa kocha wa klabu ya Siena ya Italia.

    No comments:

    Post a Comment

    VIDEO MPYA

    UMBEA MTUPUU

    MAPENZI