• Seynation Updates

    Saturday 11 June 2016

    Euro2016: Ufaransa yaishinda Romania

    Timu ya taifa ya soka nchini Ufaransa imeshinda mechi ya ufunguzi wa dimba la kombe la bara Ulaya baada ya kuinyuka Romania, mabao 2-1, katika uwanja wa Stade de France mjini Paris.
    Dimitri Payet wa Ufaransa ambaye anaichezea klabu ya West Ham nchini Uingereza alifunga bao la ushindi katika muda wa lala salama.
    Mshambuliaji wa Ufaransa Olivier Giroud alifunga bao la kwanza kwa kichwa muda mfupi tu baada ya kipindi cha pili kung'oa nanga, na baadaye Romania wakazawazisha kwa mkwaju wa penalti kutoka kwa Bogdan Stancu.
    Image copyrightGETTY
    Image captionEuro2016
    Usalama umeimarishwa mjini Paris na haswa karibu na uwanja wa Stade de France, ambapo shambulizi baya la kigaidi lilitekelezwa mwaka ulopita.

    No comments:

    Post a Comment

    VIDEO MPYA

    UMBEA MTUPUU

    MAPENZI