Watu 13 wamepoteza maisha na wengine 10 kujeruhiwa kwenye ajali basi la Super Shem lililogongana na daladala linalofanya safari zake Nyegezi na Shilima kwenye eneo la Hungumalwa mkoani Mwanza alfajiri ya leo.
Basi la Super Shem lilikuwa likitokea mkoani Mbeya kuelekea Mwanza, liligongana na daladala hiyo ambayo iliingia kwenye barabara kubwa bila ya kujua kuwa nyuma yake basi hilo linakuja kwa mwendo kasi.
Abiria wanaodaiwa kupoteza maisha na kujeruhiwa zaidi ni wale walikuwa kwenye daladala .
Hii ni ajali kubwa ya pili inayohusisha basi la abiria kutokea ndani ya wiki hii ukiacha ile iliyotokea mkoani Njombe na kuua watu 12 siku mbili zilizopita.
Picha: Michuzi
Hizi ni picha zingine za ajali hiyo.
No comments:
Post a Comment