• Seynation Updates

    Tuesday 27 December 2016

    Kocha wa zamani wa Man United achaguliwa kuifundisha KRC Genk ya Samatta

    Klabu ya soka ya KRC Genk ya Ubelgiji, imemtangaza kocha wa zamani wa Manchester United Albert Stuivenberg kuwa kocha mpya atakayeifundisha timu hiyo.

    Albert Stuivenberg (kushoto) akiwa na Van Gaal pamoja na Ryan Giggs
    Stuivenberg aliwahi kuwa kocha msaidizi wa Louis Van Gaal kwenye timu ya United kwa misimu miwili kuanzia 2014 mpaka Juni 2016 na kufanikiwa kushinda kombe la FA msimu uliopita. Kocha huyo ambaye ni raia wa Uholanzi anachukuwa mikoba ya kuifundisha timu hiyo kutoka kwa Peter Maes ambaye ametimuliwa kutokana na kuwa na matokeo mabaya kwenye timu hiyo.

    No comments:

    Post a Comment

    VIDEO MPYA

    UMBEA MTUPUU

    MAPENZI