• Seynation Updates

    Tuesday 7 March 2017

    Yanga yailaza Kiluvya United mabao 6-1, yatinga robo fainali.

    Klabu ya Yanga, imetinga katika hatua ya robo fainali ya michuano hiyo kwa msimu huu kwa kishindo baada ya kuishindilia Kiluvya United mabao 6-1, katika dimba la Uhuru Dar es Salaam.














    Katika mchezo huo ambo Yanga haikukumbana na ushindani wowote na kufanikiwa kutawala mchezo kwa zaidi ya asilimia 70 kwa 30, imeanza kujipigia katika dakika ya 11 kupitia kwa Geofrey Mwashiuya, kabla ya Mzambia Obrey Chirwa kupachika la pili dakika ya 22, na Kiluvya kupata bao lao dakika ya 40 kupitia kwa Edgar Mfumakule, ambapo hadi mapumziko Yanga ikaondoka ikiwa mbele kwa mabao 2-1.
    Kipindi cha pili, Chirwa ambaye alikuwa na mchezo mzuri zaidi siku ya leo, alifanikiwa kuongeza mabao mawili, dakika ya 48 na dakika ya 70, huku Juma Mahadhi akipiga la 5 dakika ya 74, kabla ya Chirwa tena kuhitimisha sherehe ya mabao dakika ya 87 kwa kufunga bao la sita, likiwa ni bao lake la nne katika mchezo wa leo na kuondoka na mpira.
    Baada ya matokeo hayo sasa Yanga itakutana na Wajelajela, Tanzania Prisons katika dimba la Taifa jijini Dar es Salaam ikiwa ni hatua ya robo fainali kwa mujibu wa ratiba iliyotangazwa leo.

    Jiunge na SeyNation

    No comments:

    Post a Comment

    VIDEO MPYA

    UMBEA MTUPUU

    MAPENZI