• Seynation Updates

    Sunday 23 April 2017

    Chelsea haooo Wembley wanamsubiri Arsenal au Man City. Inbox x



    Alianza Willian dakika ya tano tu ya mchezo kuanza kucheka na nyavu za Tottenham Hotspur kwa mkwaju wa faulu na kuifanya Chelsea kutangulia kwa bao moja kwa sifuri.
    Baadae Harry Kane aliisawazishia Chelsea na watu kuona kama kipindi cha kwanza kinaweza kuisha kwa sare ya bao moja kwa moja lakini Chelsea walizawadiwa penati na Willian tena akafunga la pili na kwenda mapumziko kwa matokeo ya mbili kwa moja.
    Kipindi cha pili Delle Ali aliisawazishia Tottenham Hotspur lakini mabadiliko aliyoyafanya Antonio Conte ya kumuingiza Eden Hazard yalibadilisha kabisa matokeo ya mchezo huo.
    Dakika ya 75 Eden Hazard aliifungia Chelsea bao la tatu kabla ya kuasist bao la nne lililofungwa na Nemanja Matic na kuufanya mchezo huo kuisha kwa matokeo ya bao nne kwa mbili.
    Kwa matokeo hayo Chelse imetinga fainali ya FA itakayopigwa baadae mwezi ujao katika uwanja wa Wembley huku wakimsubiri mshindi wa mchezo kati ya Arsenal na Man City utakaopigwa siku ya Jumapili.

    VIDEO MPYA

    UMBEA MTUPUU

    MAPENZI