• Seynation Updates

    Monday 10 April 2017

    Kauli ya Halima Mdee Baada ya Askofu Gwajima Kumtaka Amuombe Radhi Spika wa Bunge

    Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Dr. Josephat Gwajima jana  alijitokeza hadharani mbele ya waumini wa kanisa lake na kumtaka Halima Mdee Mbunge wa CHADEMA kumuomba radhi Spika wa Bunge Job Ndugai kwa maelezo kuwa alimtukana. Gwajima alisema, kama hatafanya hivyo, basi ataitumia Jumapili Ijayo 'kumchapa' Hadharani

     Kutokana na madai hayo, Halima Mdee amejitokeza hadharani na kumjibu Gwajima

    "Namuheshimu sana Mch. Gwajima,sitajibizana nae kwenye mitandao. Niweke rekodi sawa sijamtukana na wala sitarajii kumkosea heshima Spika.

    "Hayo ya J2 namwachia yeye! Yangu na yaliyojiri Bungeni.. Najua jinsi ya kuyahandle. Yawezekana yalishamalizwa kabla ya Ibada yake LEO."
    Namuheshimu sana Mch.Gwajima,sitajibizana nae kwenye mitandao. Niweke rekodi sawa sijamtukana na wala sitarajii kumkosea heshima Spika. https://twitter.com/mitandaonblog/status/851079630094299136 

    Hayo ya J2 namwachia yeye! Yangu na yaliyojiri Bungeni.. Najua jinsi ya kuyahandle. Yawezekana yalishamalizwa kabla ya Ibada yake LEO. https://twitter.com/mitandaonblog/status/851079630094299136 

    No comments:

    Post a Comment

    VIDEO MPYA

    UMBEA MTUPUU

    MAPENZI