Mkali wa muziki wa Singeli Bongo, Msaga Sumu anatarajia kuweka rekodi ya kuwa msanii wa kwanza wa muziki huo kutoa albamu.
Muimbaji huyo amesema albamu hiyo inakwenda kwa jina la Mwanaume Mashine na itatoka December 26 mwaka huu.
Ameongeza kuwa albamu hiyo itakuwa na nyimbo 12 zenye ladha tofauti tofauti ambazo amezifanya kwa maproducer wakubwa kama Shedy Clever, Aba, Aby Dady, Mr. T Touch na wengineo.