Mjadala wa taarifa za kuzushiwa kifo cha Msemaji wa Simba, Haji Manara umeendelea mtandaoni huku wengine wakihoji iko wapi hiyo taarifa aliyozushiwa.
Hata hivyo, Manara alitoa ufafanuzi kuhusu taarifa hizo alizozisoma kwenye mitandao ya kijamii na kueleza kwamba si za kweli kwani ni mzima.
Manara alishangazwa na watu kusambaza uvumi huo na alisisitiza kupitia akaunti yake ya Istagram kuwa yeye ni mzima kabisa.
Alisema kwamba taarifa hizo ziliwafikia ndugu zake na kuwashtua lakini hazina ukweli.