• Seynation Updates

    Thursday 25 January 2018

    Maneno ya Arsene Wenger kwa Alexis Sanchez.


    Meneja wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amesema kwa sasa mambo ya usajili wa Alexis Sanchez yameshapita ndani ya timu hiyo.
    Sanchez amekamilisha dili lake la kujiunga na Manchester United huku likimuhusisha Henrikh Mkhitaryan kuhamia Emirates mwanzoni mwa wiki hii.
    Kufuatia ushindi dhidi ya Chelsea katika michuano ya Carabao Cup hapo jana siku ya Jumatano Wenger akizungumza na vyombo vya habari juu ya uhamisho wa Sanchez amesema kuwa “Tumepoteza mchezaji bora lakini kama timu kunahaja ya kuendelea nayale muhimu ili kutopoteza muelekeo wetu,” amesema Wenger.
    “Kwa sasa tunafahamu tunapaswa kuendelea mbele sote kwa pamoja kujipatia muda.”
    Kikosi cha Wenger kimefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya michuano ya Carabao Cup na kutarajiwa kucheza na Manchester City baada ya kuifunga timu ya Chelsea hatua ya nusu fainali.

    No comments:

    Post a Comment

    VIDEO MPYA

    UMBEA MTUPUU

    MAPENZI