• Seynation Updates

    Thursday 25 January 2018

    Mwanafunzi amnyonga mpenziwe Guest

    Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) aliyetambulika kwa jina la Mwita Marwa kwenye miaka (30) anatuhumiwa kufanya mauaji kwa kumnyonga mpaka kufa mpenzi wake Kibua Adam (39) mkoani Morogoro.


    Akiongea na www.eatv.tv Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mpaka sasa jeshi la polisi linaendelea kumtafuta mtuhumiwa.
    "Mpaka sasa zipo tetesi tu za hapa na pale hatuwezi kujua sababu kubwa iliyopelekea kijana huyo kufanya jambo hilo, kwani yeye alimchukua huyo mwanamke akampeleka guest na kunyonga huko mpaka akafa" alisema Matei 
    Kamanda Matei anadai jeshi la polisi walipopata taarifa za kunyongwa mwanamke huyo alifika katika guest hiyo na kuukuta mwili wa mwanamke huyo na kuondoka nao, lakini mpaka sasa mwanafunzi ambaye anatuhumiwa kufanya mauaji hayo hajapatikana na jeshi la polisi linaendelea kumtafuta.

    No comments:

    Post a Comment

    VIDEO MPYA

    UMBEA MTUPUU

    MAPENZI