Kupitia ukurasa wa Instagram Msanii katika lebo ya WCB Rayvanny, amefunguka makubwa juu ya Diamond Platnumz na mahasimu wake. Ijulikane kuwa Diamond Platnumz hana mahusiano mazuri na baadhi ya Media kwa Sasa, na pia mahusiano kati yake na Wizara ya Habari & Sanaa si mazuri kutookana na mashambulizi aliyoyatoa juu ya Naibu waziri wa Wizara husika. SOMA KAULI TATA ZA DIAMOND KWA BASATA.
Kutokana na hayo yote yaliyo jiri Rayvanny ndie msanii wa kwanza kutoka WCB kumtia moyo na kuungana na Diamond katika mpambano huu mkali . Rayvanny aliweza kuandika kama ifuatavyo.
- ''Kuna Vitu Pengine Unaweza Ukawa Unapatia Au Vingine Unakosea Sitaki Kuongelea Hilo Sababu we nawe Ni Binadamu. ILA KWENYE KUSEMA UKWELI NITASEMA!!!! Si kwa Sababu wewe Ni boss Wangu Hapana!!! Ila Mara Nyingi Thamani Ya mtu Na Umuhimu Wa Mtu wengi Wanaujua Akishaondoka.... MZIKI NI KAZI NA NI AJIRA Namaanisha Kuna Familia Nyingi Zinaishi kupitia Huu huu mziki. DIAMOND KATIKA WASANII WOOOTE Umekua chachu Ya Kuongeza Thamani Ya Muziki Nakupitia wewe naamini Wengi Wanafanikiwa.... KUJITOA KWAKO, KUAMINI KATIKA UMOJA NA PIA KUTHUBUTU Ndiko kunafanya Unafanikiwa.... USHAAMBIWA HUJUI KUIMBA ila ukaimba ukafanikiwa... USHAAMBIWA UNAVIMBA UNAIGIZA MAISHA Lakini sasa Unayaishi hayo Maisha... Hakuna Anaefanikiwa Akakosa maadui ndivyo Dunia Ilivyo .. MIMI ULINISAIDIA ULIJUA SHIDA ZANGU Naamini Mungu Alikutumia wewe Ukawe Mkombozi Wangu ....... KWAIO KUMBUKA ( ILI MBEGU IOTE LAZIMA IOZE ) SINA MUDA KUMSEMA MTU ILA NAKUPA MOYO FANYA KAZI SIMBA....... kama Wewe Unaamini Katika Upendo Na sio Chuki, Vita Na Matusi JUST COMMENT ( LOVE )" Aliandika Rayvanny
Kama una habari au tukio lolote tutumie kwa WhatsApp 0684-224-468
Kwa Matangazo tucheki kwa WhatsApp 0684-224-468
No comments:
Post a Comment