• Seynation Updates

    Monday 28 May 2018

    KIM JONG MACHO KWA MACHO NA TRUMP...



    KIONGOZI wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un amesema nia yake ya kukutana na Rais wa Marekani Donald Trump ili kuzungumza na kufikia makubaliano iko palepale licha ya kauli yake aliyoitoa hivi karibuni iliyodhoofisha mpango huo.
    Kim Jong-un amesema hayo baada ya mkutano wake wa kushtukiza wa juzi Jumamosi na Rais wa Korea Kusini, Moon Jae-in.
    Trump alisitisha mkutano uliopangwa kufanyika Juni, 12 mwaka huu kuzungumzia mpango wa nuklia wa Korea Kaskazini, lakini juzi Jumamosi alibadili maamuzi yake na kusema kuwa mambo yanaendelea vizuri kuelekea mkutano huo.
    Imeelezwa kwamba, Balozi wa zamani wa Marekani nchini Korea Kusini, Sung Kim, atafanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Korea Kaskazini kuhusu maandalizi ya mkutano, vyombo vya habari vya Marekani na Korea Kusini vimeeleza.
    Mkutano huo ni matunda ya jitihada za kidiplomasia ambazo zilianza mwaka huu kujaribu kuondoa hali ya msuguano uliohofiwa kugeuka kuwa makabiliano ya kijeshi kati ya Korea Kaskazini, Korea Kusini na Marekani.
    Source:BBC.


    Usikose habari zaidi Tufuatilie Instagram @seynation na INSTALL APP YETU BOFYA HAPA

    No comments:

    Post a Comment

    VIDEO MPYA

    UMBEA MTUPUU

    MAPENZI