Hitmaker wa Ngoma ya TAGI UBAVU Bill Nass, amefunguka kwa mara ya kwanza tangu kusambaa kwa video yake akiwa na NANDY, Bill Nass ameyabainisha hayo kwenye kipindi Cha Kikaangoni.
“Kuna wimbo tumefanya pamoja, wimbo umefanywa chini ya S2kizzy hivyo naamini muda ukifika utatoka tu ila nachojua ni wimbo mkali, kuhusu jambo ambalo limetokea,” amesema Bill.
Rapper huyo ameongeza, “Kuhusu mimi na yeye tayari nilishaomba radhi kwa wananchi na sasa maisha ya kawaida yanaendelea, hivyo hatuna tofauti yoyote ile kwa kuwa yule ni rafiki yangu na nina iheshimu sana familia yake akiwa pamoja na mama yake kwa kuwa ni mtu ambaye amekuwa akijitoa sana kusupport kazi za mwanae.”
SOMA HABARI KUPITIA INSTAGRAM ACCOUNT YETU @seynation
Usikose habari zaidi Tufuatilie Instagram @seynation na INSTALL APP YETU BOFYA HAPA
No comments:
Post a Comment