• Seynation Updates

    Monday 13 November 2017

    United hawamtaki Bale wala Griezman bali huyu ndio nyota wanayejipanga kuvunja kibubu kwa ajili yake



    Manchester United walikosa amani sana baada ya dili la uhamisho wa nyota wa Ufaransa Antoine Griezman ambalo walipambana kwa muda mrefu sana lakini ikashindikana dakika za mwisho.
    Baada ya hapo United walimnunua Lukaku lakini ikatajwa kwamba bado wanatega kuhusu Griezman na pia wanaangalia kwa ukaribu maendeleo ya nyota wa Real Madrid Gareth Bale ambaye anaandwamwa na majeruhi.
    Lakini sasa yameibuka mengine kwani United wanaonekana wako serious kwenye uhamisho wa nyota kinda wa Real Madrid ambaye siku za karibuni amekuwa gumzo kubwa katika ulimwengu wa soka Marco Asensio.
    Inasemekana kwamba United wanataka kuvunja rekodi ya usajili tena klabuni hapo kwa kutoa kiasi cha £170m na mshahara wa £461,000 kwa ajili ya kumnunua Asensio katika dirisha lijalo la usajili.
    Habari zaidi zinadai kwamba Asensio na Mourinho wameshawahi kufanya mazungumzo na kama dili hilo likifanikiwa baasi Asensio anaweza kusaini mkataba wa miaka 5 kuitumikia United.
    Manchester United wanajipanga kutumka tena kiasi kikubwa zaidi cha pesa katika dirisha kubwa la usajili mwakani na sasa Asensio naye anaingia kwenye rada za Mashetani hao wekundu.

    VIDEO MPYA

    UMBEA MTUPUU

    MAPENZI