• Seynation Updates

    Wednesday 11 January 2017

    Jerry Muro Adai Simba Wasinge Shinda Wangeweza Vunja Hata Muungano



    Baada ya klabu ya Yanga kuambulia kichapo cha penati nne kwa mbili katika mchezo wa nusu fainali ya kombe la Mapinduzi Jumanne hii, aliyekuwa afisa habari wa klabu ya Young Africans Jerry Muro ambaye kwa sasa bado anatumikia adhabu ya kufungiwa na TFF, amewatupia dongo watani wake wa klabu ya Simba.


    Mashabiki wa Klabu ya Simba amekuwa wakitaniwa mara kwa mara na mashabiki wa Yanga baada ya kufanya tukio la kuvunja viti katika uwanja wa Taifa wakati wa kicheza na watani wao wajadi Yanga.

    Muro amerusha kijembe hicho kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram kwa kuandika

    ‘Sikilizeni nyinyi…Bora hata Simba mmeshinda, maana mlivyo watata mngeweza hata vunja Muungano’

    Watani hao wa jadi wanatarajiwa kukutana tena katika mzunguko wa pili wa ligi kuu wa Tanzania bara ambayo sasa hivi imesimama kwa muda kupisha michuano ya kombe la Mapinduzi. 


    Ili ujue kinachoendelea Mtu wangu usiache kukaa karibu yangu kwenye   FACEBOOK na  INSTAGRAM  @seynation ili niwe nakutumia kila kinachoonifikia.


    No comments:

    Post a Comment

    VIDEO MPYA

    UMBEA MTUPUU

    MAPENZI