• Seynation Updates

    Tuesday 10 January 2017

    MAABARA YA HISABATI 'MATHEMATICS' ILIYOZINDULIWA NA NDALICHAKO.

      Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amezindua maabara ya somo la Hisabati iliyopewa kwa jina la ‘Hey Mathematics Programme’ na kusema itawezesha wanafunzi kufurahia na kuona urahisi wa kusoma somo hilo.Akizindua maabara hiyo jijini Dar es Salaam, Waziri huyo amesema mpango huo utasaidia kujenga msingi mzuri wa somo la Hisabati kwa wanafunzi.
    “Kama tunavyojua watoto wetu wanapenda mambo ya teknolojia, unakuta mara nyingi wako kwenye simu wako kwenye komputa kwahiyo ni mfumo ambao unaendana na vitu ambavyo vinawavutia vijana. Ni dhahiri kwamba kama una utiwa na kitu uwezekano wa kukifanya vizuri ni mkubwa kuliko jambo ambalo halikuvutii,’ alisema Ndalichako.
    SOURCE: BONGO5,COM


    Ili ujue kinachoendelea Mtu wangu usiache kukaa karibu yangu kwenye   FACEBOOK na  INSTAGRAM  @seynation ili niwe nakutumia kila kinachoonifikia.

    No comments:

    Post a Comment

    VIDEO MPYA

    UMBEA MTUPUU

    MAPENZI