Mwanamke ambaye anatarajiwa kuwa mke wa saba wa aliyekuwa rais wa Afrika kusini,Jacob Zuma amelazimishwa kujiuzulu ajira yake ya ukuu wa asasi isiyokuwa ya kiserikali na chombo cha habari cha nchini humo, asasi iliyokuwa ikijishighulisha na maswala ya kupinga Mabinti kuolewa na Vizee
Nonkanyiso Conco ambaye ana mahusiano ya kimapenzi na bwana Zuma ambaye amemzidi umri wa miaka 52
Wakati huo yuko kwenye asasi inayohamasisha kampeni ya kuwawezesha mabinti wadogo katika maisha yao ya kila siku na kuacha kuwategemea wanaume wenye umri mkubwa.
Bi.Conco mwenye miaka 24 amejifungua mtoto wa Zuma katika hospitali ya binafsi iliyoko mjini Durban.
Zuma kwa sasa ana umri wa miaka 76,ana wake wanne na mwingine mmoja waliachana na mke wa sita alijiua mwaka 200 pamoja na watoto ishirini.
No comments:
Post a Comment