• Seynation Updates

    Saturday 26 May 2018

    Emmanuel Mbasha apangua tuhuma za kuazima magari

    Msanii wa muziki wa Injili Bongo, Emmanuel Mbasha amejibu kuhusu tuhuma za kuazima magari ya watu kwa ajili kupiga picha ili kujionyesha katika mitandao.


    Muimbaji huyo amesema tuhuma hizo hazina ukweli wowote kwani kazi zake anazozifanya zinatosha kumuingiza kipato cha kuweza kumiliki magari kadhaa.
    “Hamna, mimi huwa siazimi magari, yote niliyona ni ya kwangu, ninatumia gari zangu na watu wa karibu yangu wanafahamu mimi ni mfanyabiashara, ninaimba Gospel na nina kipato cha kufanya mambo yangu yote ya unayoyaona,” Mbasha ameiambia Bongo5.
    Ameongeza kuwa kwa sasa anamiliki magari mawili. Wimbo wa mwisho Mbasha kutoa ni Hallelujah ambao amemshirikisha Hondwa, wimbo huo ulitoka October 2017.
    Usikose habari zaidi Tufuatilie Instagram @seynation na INSTALL APP YETU BOFYA HAPA

    No comments:

    Post a Comment

    VIDEO MPYA

    UMBEA MTUPUU

    MAPENZI