• Seynation Updates

    Saturday 9 June 2018

    ZADI YA WATU 250 WILAYANI NGARA-KAGERA WAATHIRIKA NA KUJAA KWA MTO RUVUBU

    34462653_1882378108468757_5316126462460297216_n
    Muonekano wa maji ya mto ruvubu yakiwa yamejaa kupita kiasi  na kusababisha  Kivuko cha MV RUVUBU kushindwa kufanya kazi yake kama kawaida  ambapo Wananchi mbalimbali  hukitumia kuvuka kama anaenda mpaka wa Rusumo kutalii au kufatilia mambo mbalimbali yaliyopo,yapo na yajayo hasa ukizingatia ni Mpakani mwa Tanzaniana Rwanda.

    34461549_1882378055135429_767325744568205312_n
    Wananchi wa kijiji cha Kyenda kata ya Murukulazo wilayani Ngara mkoani Kagera wameiomba serikali kuchukua hatua juu ya maji yaliyojaa mto ruvubu na kufurika kwenye mashamba yao.

     Wakizungumza na Radio Kwizera Kijijini hapo wamesema hali ya mavuno kwa msimu huu ni ngumu kwao baada ya maji kufurika kwenye mto huo na mto Kagera baada ya kuzibwa na mradi wa umeme Rusumo NELSAP.

    Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji hicho Bw Ferdinand Festo Masenge amesema mpaka sasa zaidi ya Wananchi 300 wamekwisha athirika na maji hayo ambayo yameharibu kiasi kikubwa cha mazao mashambani.

    Naye Diwani wa Kata ya Murukulazo ( CCM ) Bw Mukiza Byamungu amesema mbali na athari za Kilimo lakini pia Sekta ya Afya, Elimu na Biashara zimeharibiwa kwa kiasi kikubwa kwakuwa baadhi ya walimu, wauuguzi na wanafunzi hutegemea kivuko ambacho kwasasa hakina uwezo wa kutoa huduma.

    CREDITS: MWANA WA MAKONDA


    Usikose habari zaidi Tufuatilie Instagram @seynation na INSTALL APP YETU BOFYA HAPA

    No comments:

    Post a Comment

    VIDEO MPYA

    UMBEA MTUPUU

    MAPENZI